Na Barnabas Kisengi-Dodoma Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe amewataka wafanyabiashara nchini kuchangamkia fursa zilizopo ili kuweza kukuza sekta hiyo ambayo inatoa ajira na kuchangia pato la Taifa.Akizungumza katika mkutano mkuu wa mwaka wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA), baina ya sekta ya Umma na sekta binafsi uliofanyika jijini Dodoma.
Na Barnabas Kisengi-Dodoma
Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe amewataka wafanyabiashara nchini kuchangamkia fursa zilizopo ili kuweza kukuza sekta hiyo ambayo inatoa ajira na kuchangia pato la Taifa.
Akizungumza katika mkutano mkuu wa mwaka wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA), baina ya sekta ya Umma na sekta binafsi uliofanyika jijini Dodoma.
Kigahe amewataka kuendelea kuibua changamoto mbalimbali zilizopo kupitia tafiti wanazozifanya ili kuweza kuboresha mazingira ya biashara hizo .
Kwa upande wake Rais wa wafanyabiashara, viwanda na kilimo Tanzania, Paul Koyi, amesema watatumia fursa waliyopewa na Rais Samia katika kupanua wigo wa biashara kwa kuhakikisha zinafanyika kimataifa, huku akisisitiza uaminifu kama nguzo kuu ya biashara.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *