Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewasili Nchini Burundi kwa ajili ya kushiriki Sherehe za miaka 60 ya Jamhuri ya Burundi zitakazofanyika kesho 01 Julai nchini humo. Rais Dk. Mwinyi akiwa ameambatana na Mkewe Mama Mariam Mwinyi,Mawaziri wa SMT na SMZ na Viongozi wa Taasisi mbalimbali,katika Uwanja wa
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewasili Nchini Burundi kwa ajili ya kushiriki Sherehe za miaka 60 ya Jamhuri ya Burundi zitakazofanyika kesho 01 Julai nchini humo.
Rais Dk. Mwinyi akiwa ameambatana na Mkewe Mama Mariam Mwinyi,Mawaziri wa SMT na SMZ na Viongozi wa Taasisi mbalimbali,katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Melchior Ndadaye jijini Bujumbura wamepokelewa na Viongozi mbalimbali wa ngazi za juu wa Burundi wakiongozwa na Waziri anaeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki ,Vijana,Michezo na Utamaduni Balozi Ezechiel Nibigira pamoja na Balozi wa Tanzania nchini humo Dkt.Jilly E.Maleko
Rais Dk.Mwinyi alipita katika ya Gwaride maalumu la Heshima lililoandaliwa kwa ajili yake kiwanjani hapo.
Katika sherehe hizo za miaka 60 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi,Rais Dk.Hussein Ali Mwinyi anamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.
Rais Dk.Hussein Ali Mwinyi pia anatarajiwa kukutana na kufanya Mazungumzo na Mwenyeji wake Rais wa Burundi Evariste Ndayeshimiye katika ikulu ya Burundi iliyopo jijini Bujumbura .
Taifa la Burundi linaadhimisha kumbukumbu ya miaka 60 tokea taifa hilo lilipojipatia Uhuru wake kutoka kwa wakoloni wa Ubelgiji Julai 1, 1962.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *