WAZIRI AWESO AZITAKA MAMLAKA ZA MAJI KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAJI KWA WANANCHI

WAZIRI AWESO AZITAKA MAMLAKA ZA MAJI KUTATUA CHANGAMOTO ZA MAJI KWA WANANCHI

Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso amewataka Wakurugenzi watendaji wa Mamlaka za MajiSafi na Usafi wa Mazingira nchini kushughulikia changamoto za wananchi zinazohusiana na upatikanaji wa huduma bora ya Maji. Ameyasema haya wakati akifunga kikao kazi cha Wakurugenzi Watendaji wa Majisafi na Usafi wa Mazingira nchini kilichofanyika mkoani Morogoro. Aidha Waziri Aweso ameeleza kuwa Wakurugenzi wa

Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso amewataka Wakurugenzi watendaji wa Mamlaka za MajiSafi na Usafi wa Mazingira nchini kushughulikia changamoto za wananchi zinazohusiana na upatikanaji wa huduma bora ya Maji.

Ameyasema haya wakati akifunga kikao kazi cha Wakurugenzi Watendaji wa Majisafi na Usafi wa Mazingira nchini kilichofanyika mkoani Morogoro.


Aidha Waziri Aweso ameeleza kuwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Maji wawe karibu na jamii na zaidi wawe na Utamaduni mzuri wa kupokea taarifa na kuzifanyia kazi pamoja na kutoa taarifa kwa wananchi pale inapobidi ili kutengeneza daraja zuri la mawasiliano kati yao na wananchi.


Pamoja na haya amezitaka mamlaka ambazo zinaendelea na Utekelezaji wa Miradi zihakikishe zinakamilisha miradi hii kwa haraka kwani baada ya Bunge ataanza ziara rasmi kupita maeneo yote nchini kufatilia utekelezaji wa Miradi ya Maj.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »