KANISA LA MORAVIAN LAISHAURI SERIKALI KUWAWEKEA MAZINGIRA RAFIKI WANAFUNZI.

KANISA LA MORAVIAN LAISHAURI SERIKALI KUWAWEKEA MAZINGIRA RAFIKI WANAFUNZI.

Na; Emesto Eliudy, Dar Es Salaam Serikali kupitia Wizara ya elimu nchini, imeshauriwa kuandaa mitaala rafiki Kwa ajili ya masomo Kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari ili kuwajengea uwezo mkubwa na uelewa mpana wa elimu wanafunzi hao. Ushauri huo umetolewa jijini Dar Es Salam na Mchungaji wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la

Na; Emesto Eliudy, Dar Es Salaam

Serikali kupitia Wizara ya elimu nchini, imeshauriwa kuandaa mitaala rafiki Kwa ajili ya masomo Kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari ili kuwajengea uwezo mkubwa na uelewa mpana wa elimu wanafunzi hao.

Ushauri huo umetolewa jijini Dar Es Salam na Mchungaji wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Mashariki Ushirika wa Tabata, Mch. Emmanuel Mahembo baada ya kumaliza ibada ya kuombea Msimu mpya kwa wanafunzi wanaorudi shuleni ambapo amesema Kuwa Serikali Ina wajibu wa kuboresha miundombinu ya shule ili wanafunzi wasome katika mazingira rafiki na kuwaongezea ufaulu wanafunzi hao.

Mchungaji wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Mashariki Ushirika wa Tabata, Mch. Emmanuel Mahembo

Akizungumza Kwa niaba ya wazazi, Atuganile Mjwanga, amesema kuwa wazazi wamekuwa na majukumu mengi kiasi ambacho wanasahau kuwaombea watoto ambao wapo kwenye shule mbalimbali hivyo amewataka wazazi kutenga muda wa kuwafuatilia watoto wao.

Mchungaji wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Mashariki Ushirika wa Tabata, mch. Emmanuel Mahembo akiwaombea Wanafunzi waliohudhuria ibada Maalum ya Maombi ya muhula mpya wa masomo Kwa wanafunzi iliyofanyika Katika Kanisa Hilo Ushirika wa Tabata.

Kwa upande wake Daniel Hamphrey ambaye ni mwanafunzi wa kidato Cha pili amelishukuru Kanisa Hilo Kwa kuona umuhimu wa kuwaombea huku akiwasihi wanafunzi kumtegemea Mungu Zaidi katika masomo yao.

Wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali waliojitokeza kwenye Ibada ya Maombi Maalum ya muhula mpya wa masomo yao iliyofanyika Katika Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Mashariki Ushirika wa Tabata
Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »