Na Mwandishi Wetu Dar es salaam Timu ya Wataalam wa Mawasiliano na Uhusiano wa Taasisi zilizoko chini ya Wizara ya Afya mkoa wa Dar es salaam leo wametoa elimu kwa umma juu ya umuhimu wa Bima ya Afya kwa wote kwa wajumbe wa kamati ya Afya ya Mkoa Dar es Salaam (RHMT). Wajumbe wa kamati
Na Mwandishi Wetu Dar es salaam
Timu ya Wataalam wa Mawasiliano na Uhusiano wa Taasisi zilizoko chini ya Wizara ya Afya mkoa wa Dar es salaam leo wametoa elimu kwa umma juu ya umuhimu wa Bima ya Afya kwa wote kwa wajumbe wa kamati ya Afya ya Mkoa Dar es Salaam (RHMT).
Wajumbe wa kamati hiyo waliongozwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Rashid Mfaume.
Baada ya wasilisho wajumbe walipata nafasi ya kuuliza maswali mbalimbali ili kuongeza uelewa ambapo timu ilifafanua hoja mbalimbali kwa ushirikiano mkubwa.
Elimu hiyo itaendelea kwa wadau wote wa ngazi za mbalimbali.
Wajumbe wa kamati hiyo ya Afya ya Mkoa wa Dar es Wameahidi kuwa mabalozi wazuri katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa bima ya afya kwa wote.
Taasisi zilizoshiriki ni JKCI, Muhimbili, GCLA, TFNC, ORCI, MSD, TMDA, MOI
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *