Waziri wa Maji Jumaa Aweso amefungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Sekta ya Maji na amewataka Watendaji Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maji kufanya kazi kwa kasi, uadilifu na uwajibikaji ili lengo la serikali la kutoa huduma bora ya majisafi lifanikiwe hasa akisisitiza kufanyiwa kazi eneo la Takwimu. Waziri Aweso ameainisha kuwa
Waziri wa Maji Jumaa Aweso amefungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Sekta ya Maji na amewataka Watendaji Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maji kufanya kazi kwa kasi, uadilifu na uwajibikaji ili lengo la serikali la kutoa huduma bora ya majisafi lifanikiwe hasa akisisitiza kufanyiwa kazi eneo la Takwimu.
Waziri Aweso ameainisha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt SAMIA SULUH HASSAN ameonesha nia ya dhati ya kusaidia juhudi za Wizara ya Maji kufikisha huduma ya maji kwa Watanzania,hivyo watendaji wa Wizara wanajukumu la kuhakikisha wanaungana naye kwa kuhakikisha wanakuwa waadilifu na kuratibu matumizi yaliyokusudiwa ya fedha katika miradi yote ya Maji inayotekelezwa hapa nchini
.
Aidha Waziri wa Maji Jumaa Aweso ametoa tathmini ya wapi sekta ya Maji imetoka, wapi ilipo sasa na mipango ya wapi inaelekea akiyachambua maeneo yalio vizuri na maeneo yenye changamoto na yanayotakiwa kufanyiwa kazi pia akiwapongeza watendaji wa sekta ya Maji kwa kuwa mstari wa mbele kusimamia mageuzi ambayo yamewezesha utekelezaji wa miradi ya maji.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *