Kambi za matibabu zitasaidia kuondoa matatizo ya Afya kwa wananchi.

Kambi za matibabu zitasaidia kuondoa matatizo ya Afya kwa wananchi.

Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mke wa Rais wa Zanzibar, Mama Mariam Mwinyi amesema hatua ya wadau wa afya kuweka kambi za matibabu Zanzibar, itasaidia kuondoa matatizo ya afya yanayowakabili wananchi. Akizungumza na ujumbe wa watendaji wa hospitali ya Kitengule, kutoka Dar es Salaam, ofisini kwake Migombani

Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mke wa Rais wa Zanzibar, Mama Mariam Mwinyi amesema hatua ya wadau wa afya kuweka kambi za matibabu Zanzibar, itasaidia kuondoa matatizo ya afya yanayowakabili wananchi.

Akizungumza na ujumbe wa watendaji wa hospitali ya Kitengule, kutoka Dar es Salaam, ofisini kwake Migombani Mkoa wa Mjini Magharibi, Mama Mariam amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa mikakati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwafikishia huduma za matibabu wananchi wake maeneo karibu na makaazi yao.

Amesema hatua hiyo pia inaonesha kuwajali wananchi kwenye suala zima la afya na kueleza kufarijika kwake baada ya watendaji hao kutambua fursa za matibabu kupitia sekta ya utalii ambapo itasaidia zaidi kuongeza idadi ya wageni kwa kuwa na uhakika wa matibu.

Mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo ya ZMBF, bi Fatma Fungo ameupongeza ujumbe huo na kuushukuru kwa kuwapatia vifaa vya kitabibu vikiwemo vya uchunguzi wa maradhi na kueleza kwamba vitasaidia kuendesha huduma za kambi za matibabu pamoja na kampeni za afya zinazoratibiwa na ofisi hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya ujumbe wa hospitali ya Kitengule, Mkurugenzi wa huduma za afya Dk. Restuta kibasa amesema, wamefurahishwa na muitikio wa wananchi waliokuja na kupata huduma zikiwemo za uchunguzi na matibabu kwa waliogunduliwa na matatizo mbali mbali.

Jumla ya wananchi 360 walifikiwa kupata huduma za matibabu kupitia kambi iliyoendeshwa na hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dar-es Salaam huko hospitali ya Kitogani Mkoa wa Kusini Unguja ambako wagonjwa wapatao 104 walipatiwa matibabu.

IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »