WATUMISHI WA UMMA JIEPUSHENI NA MIKOPO KAUSHA DAMU.

WATUMISHI WA UMMA JIEPUSHENI NA MIKOPO KAUSHA DAMU.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa  Umma na Utawala Bora Mhe.Ridhiwani Kikwete (Mb) amewatahadharisha Watumishi wa Umma kujiepusha na mikopo yenye riba kubwa maarufu kwa jina la ” Kausha Damu” huku akisisitiza kuwa mikopo ya aina  hiyo imekuwa ikidhalilisha na kutweza utu wa Watumishi katika Jamii.  Mhe.Kikwete ametoa tahadhari hiyo wakati akizungumza

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Mkoani Simiyu, ikiwa ni ziara yake ya kikazi mkoani humo ya kuzungumza na kusikiliza changamoto zinazowakabili watumishi hao. 
Sehemu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati akizungumza na wilayani humo kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa  na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya ulinzi na usalama ya Halmashauri ya Wilaya ya Busega mara baada ya kukagua zahanati iliyotekelezewa na mradi wa TASAF 

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa  Umma na Utawala Bora Mhe.Ridhiwani Kikwete (Mb) amewatahadharisha Watumishi wa Umma kujiepusha na mikopo yenye riba kubwa maarufu kwa jina la ” Kausha Damu” huku akisisitiza kuwa mikopo ya aina  hiyo imekuwa ikidhalilisha na kutweza utu wa Watumishi katika Jamii. 

Mhe.Kikwete ametoa tahadhari hiyo wakati akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Busega Mkoani Simiyu wakati akihitimisha ziara yake aliyoianza mapema wiki hii Mkoani Mara. 

Amesema mikopo hiyo imewafanya baadhi ya watumishi wa umma   kuathirika kisaikolojia na kushindwa kufika katika vituo vya kazi na hivyo kuathiri  utoaji wa  huduma bora kwa wananchi.  

Amefafanua kuwa mikopo hiyo ambayo huchukuliwa kwenye Taasisi za Kifedha  zisizotambulika imekuwa na  riba kubwa ambayo huwapelekea Watumishi wengi kushindwa kuwasilisha  marejesho na hivyo kupelekea kuuzwa kwa  nyumba au vitu vya thamani  wanavyo vimiliki.

 Kufuatia hatua hiyo, Mhe.Kikwete amewataka Watumishi kuanza kutumia Mfumo mpya wa kieletroniki wa kukopa (e-loans)  ulioanza kutumika kuanzia Septemba 1, 2023  ambao unamuwezesha Mtumishi wa Umma kuomba mkopo pasipo kufika kwenye Taasisi ya Kifedha au Tawi la Benki. 

Amesema mfumo huo umeanzishwa na Ofisi ya Rais –  UTUMISHI na Utawala Bora ili kumsaidia Mtumishi wa Umma  kupata mikopo katika Taasisi za Kifedha zinazotambulika na Mwajiri ili kumuepusha  Mtumishi  kukopa sehemu ambazo humpeleka Mtumishi   kunyang’anywa kadi ya Benki.

 Aidha, Mhe.Kikwete amewataka watumishi hao kujenga nidhamu ya matumizi ya pesa wanazopata kwa ajili ya mustakabali wa maisha yao ya  baadaye baada ya kustaafu. 

Amewasihi kujiwekea malengo ya kujiandaa kustaafu kuanzia leo ili wasije kuwa wateja wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaoratibiwa na Mfuko wa Kuendeleza Jamii ( TASAF ). 

“Hakikisheni hata hela mnazozikopa mnafanya uwekezaji wa kimkakati kwa ajili ya kujitegemea kiuchumi katika siku za mbeleni” amesisitiza Mhe.Kikwete.

 Katika ziara hiyo Mhe.Kikwete mbali ya kuzungumza na watumishi wa umma katika mikoa ya Mara na Simiyu pia  amekagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na TASAF pamoja na kuzungumza na walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na TASAF.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »