WANAWAKE WAASWA KUONDOKANA NA DHANA YA MFUMO DUME IKIWA NI KUELEKEA KILELE CHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

WANAWAKE WAASWA KUONDOKANA NA DHANA YA MFUMO DUME IKIWA NI KUELEKEA KILELE CHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Katika kuelekea kilele cha sikukuu ya wanawake duniani ambayo huadhimishwa March 8, mwaka huu Serikali imesema sikukuu hizo zitaadhimishwa kwa ngazi ya mikoa ambapo kumekuwa na Kongamano lililojumuisha wanawake wa Mkoa wa Geita lililoandaliwa na FETTYFIVE kwa kushirikiana na  WAG HILL lililoafanyika leo tarehe 6/3/2021 Katoro katika ukumbi wa JJ Hotel. Katika Kongamano hilo mgeni


Katika kuelekea kilele cha sikukuu ya wanawake duniani ambayo huadhimishwa March 8, mwaka huu Serikali imesema sikukuu hizo zitaadhimishwa kwa ngazi ya mikoa ambapo kumekuwa na Kongamano lililojumuisha wanawake wa Mkoa wa Geita lililoandaliwa na FETTYFIVE kwa kushirikiana na  WAG HILL lililoafanyika leo tarehe 6/3/2021 Katoro katika ukumbi wa JJ Hotel.

Katika Kongamano hilo mgeni RASMI alikuwa KATIBU CCM WILAYA YA MBOGWE Ndg GRACE SHINDIKA ambaye aliwakumbusha Wanawake kuachana na dhana potofu kama mila na desturi zinazomwona Mwanaume pekee ndiyo anaefaa kuwa Kiongozi, Mfumo DUME katika jamii kuwa Mwanamme ni Kichwa,Rushwa ya Ngono katika kujitokeza Kugombea nafasi za Uongozi .


Shindika ameendelea Kuwaasa kinamama kuielimisha jamii juu ya hayo na kuwaomba Wanawake kuendelea kutoa elimu bora kwa watoto ambao ni taifa la kesho
Aidha shindika amewaasa wanawake kuhakikisha wanakuwa wajasili na kujitokeza katika nafasi mbalimbali za uongozi katika maeneo mbalimbali Kama taasisi binafsi, taasisi za dini serikalini na kwaenye vyama vya siasa kwani wanawake wakipata nafasi wanaweza na wanahofu ya mungu na wanawake ni wazalendo

Na Barnabas Kisengi

Geita March 6, 2021

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »