Padri Monsinyori Deogratias Hukumu Mbiku wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam afariki Dunia. Taarifa za kifo chake imetolewa na Askofu Mkuu wa Dar es Salaam, Jude Thaddaeus Ruwa’ichi. Wapendwa Mapadri, Mashemasi, Watawa na taifa lote la Mungu, Kristo. Kwa masikitiko makubwa napenda kuwataarifu juu ya kifo cha Padri wetu mpendwa Monsinyori Deogratias Hukumu Mbiku
Padri Monsinyori Deogratias Hukumu Mbiku wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam afariki Dunia. Taarifa za kifo chake imetolewa na Askofu Mkuu wa Dar es Salaam, Jude Thaddaeus Ruwa’ichi.
Wapendwa Mapadri, Mashemasi, Watawa na taifa lote la Mungu, Kristo.
Kwa masikitiko makubwa napenda kuwataarifu juu ya kifo cha Padri wetu mpendwa Monsinyori Deogratias Hukumu Mbiku wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, aliyekuwa Paroko wa Parokia ya Chuo Kikuu.
Monsinyori Mbiku amefariki leo tarehe 04 Aprili 2021 saa 12:45 jioni katika Hospitali ya Kardinali Rugambwa, Dar es Salaam, alipokuwa akitibiwa. Taarifa zaidi juu ya taratibu za Mazishi zinapangwa na tutawataarifu.
Naomba tumuombee Pumziko la Milele Mbinguni.
ASANTENI.
Jude THADDAEUS Ruwa’ichi,
Askofu Mkuu wa Dar es Salaam.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *